Uchafuzi wa mazingira unasababisha athari nyingi katika jamii. Uchafuzi huo wa mazingira unatokana na kutupa takataka ovyo katika sehemu zisizoruhusiwa kama barabarani, kwenye mazingira ya nyumba zetu na kadhalika. Wazalishaji wakubwa wa takataka ni viwanda, tasisi za elimu (shule na vyuo), hospitali, tasisi za dini n.k. Ili kuepuka athari hizo elimu ya mazingira ni muhimu sana.

Mabadiliko ya tabia ya hali ya hewa duniani ni miongoni mwa athari za uchafuzi wa mazingira. Hali ya joto imeongezeka duniani, barafu katika milima imepungua au imekwisha. Mlima Kilimanjaro kwenye miaka ya 1970 na 1980 ulikuwa umefunikwa na barafu kwa kiasi kikubwa, kwa sasa barafu imeisha. Hii imetokakana na athari za uharibifu wa mazingira. Maji katika bahari yameongezeka ina maana kina cha maji baharini kimepanda, visiwa vingine vimemezwa na bahari.

Athari nyingine ni kuibuka kwa magonjwa kama magonjwa ya ngozi na kansa. Haya yote yanatokana na maendeleo yasiyokuwa endelevu (non-sustainable development)

Tutunze mazingira kwa faida ya wote. Mazingira yatunzwe kwa kizazi hiki na kijacho. Kila mmoja akiwa mlinzi wa mwingine/mwenzake katika matumizi ya mazingira nadhani tutafanikiwa kupunguza athari za binadamu katika mazingira na kupunguza magonjwa ya mlipuko na kuyahifadhi mazingira yetu na kufurahia matunda ya mazingira mazuri kwa kizazi hiki na kijacho. Elimu ya mazingira ni muhimu kwa kila mtu.